Mkali wa muziki wa Afro Beats kutoka Tanzania mwenye makazi yake Ubelgiji, Zblack Braah amewashauri wasanii kutoka Afrika Mashariki kupeperusha kimataifa lugha ya Kiswahili baada ya kauchia Remix ya wimbo wake ‘Mtoto wa ki-afrika’ akiwa amemshirikisha Shilole.

Akizungumza na DizzimOnline akitoa sababu za kumshirikisha Shilole, ZBlack alieleza kuwa ni katika namna ya kuendelea kukuza lugha ya Kiswahili kupitia muziki kwani anaamini Mwimbaji Shilole ni kati ya wasaosikika mbali kupitia muziki wakw ambao zaidi anatumia lugha hiyo.

Katika hatua ya kukuza Kiswahili kupitia Muziki, ZBlack aliongeza kuwa lugha hiyo inakua kwa kasi kibiashara kwa nguvu ya wasanii zaidi kwa wasanii kutoka Tanzania hivyo ni jukumu la kila wasanii kuongeza bidii kuitangaza zaidi lugha hiyo katika mataifa ya mbali kupitia muziki.
Tazama Video ya Remix ya wimbo wake huo hapa chini.




