Staa wa muziki kutoka lebo ya WCB Wasafi, Rajab Abdul Kahali a.k.a Harmonize amewapa zawadi ya magari mawili ya aina moja wazazi wake.
Staa huyo mwenye umri wa miaka 25, alionesha kufanya hivyo kupitia Insta Story yake hata kuwapa uhuru kila mmoja wa kuchagua ni gari ipi atachukua.
Hatua hii imekuja, wiki chache tangu mkali huyo wa wimbo ‘Never Give Up’ amzawadie gari rafiki yake wa karibu ‘Jose Wa Mpango’ kama shukrani ya mchango wake kwenye hatua za mafanikio yake.
Yatazame Mahojiano na Jose Wa Mipango.




