Mkongwe wa Bongo Fleva, Lady JayDee amethibitisha kuwa kwenye kolabo na Msanii wa muziki kutoka lebo ya MMB, Dogo Janja.
Kolabo hiyo na Janja, Jide aliitaja kuwa ni kolabo yake ya Pili yake kushiriki kwa mwaka 2020 kwa mujibu wake kwenye ukurasa wake wa twitter.
Collabo no.2 ~ 2020 ?????
Haya mambo ndio yananipa uvivu ku release vitu vyangu pic.twitter.com/74SRYNL5li— Lady JayDee (@JideJaydee) May 8, 2020
Kwa sasa Lady Jaydee a.k.a Binti Komando anaendelea kusikika kwa uzuri kwenye wimbo ‘Kiwembe’ aliyoshirikishwa na Rapper Joh Makini.




