Msanii wa muziki wa kizazi kipya Mrlambert mzaliwa wa Tanzania, mwenye makazi yake nchini Marekani amethibitisha kuwa kwenye mpango wa maandalizi ya EP yake ya nyimbo zilizotayarishwa na mkali wa baadhi ya hit single za Diamond Platnumz, S2kizzy.
Akizungumza na Dizzim Online Mrlambert anathibitisha ujio huo baada ya kuachia video ya wimbo wake mpya ‘Shame Em’ na kueleza kuwa EP hiyo ijayo itakuwa na nyimbo zisizopungua 5.

Hata hivyo Mrlambert katika ujio huo mpya alidokeza kiasi kuwa mbali na kutayarishwa na S2Kizzy, atawashrikisha wasanii kutoka Tanzania na Jamaika kwenye EP hiyo.
Tanzana video ya wimbo wake ‘Shake Em’




