Mrembo Nayika Thongom ‘Nnayikaa’ raia wa Thailand mwenye umri wa miaka 25 aliyepata umaarufu zaidi Afrika Mashariki kwa kuwa kwenye Mahusiano ya kimapenzi na Nyota wa muziki Juma Jux, amedai kuwa ni miezi sasa yuko mbali na mpenzi wake na nam-miss’.

Nnayikaa ambaye ni mwanamitindo aliutumia Ukurasa wake wa Instagram kueleza hilo kwa lugha ya ‘ki-Thai’, ambapo alimjibu kwa kukanusha kauli ya shabiki aliyemuita mrembo huyo kuwa ni mke wa Jux.
Nnayika alimjibu shabiki huyo kuwa sio Jux kwa maana ya kuwa baada ya kuachana na Jux na kulithibitisha hilo kwa wafuatiliaji wake, Mrembo huo kwa sasa tayari ameingia kwenye mahusiano mengine na mwananume mwingine aliyehisiwa kuwa jina lake linaanza na herufi ‘A’.




