Gwiji wa Saxophone na mwimbaji mkongwe wa muziki wa dansi nchini Tanzania, Mafumu Bilal Bombenga amefariki dunia usiku wa Mei 11, 2020.
Mke wa Mafumu alithibitishia kifo chake na kusema kuwa mumewe alifariki baada ya hali yake ilibadilika ghafla ambapo aliaga dunia muda mfupi baadae.
Mafumu mbali na kushirikia kwenye bendi kadhaa kubwa nchini, ameacha ufundi wake wa kupiga Saxophone kwenye wimba wa ‘Kama Zamani’ wa Mwana Fa Ft Kilimanjaro Band, Mandojo & Domokaya.




