Msanii wa muziki kutoka nchini Marekani mzaliwa wa Tanzania, Rhino The Don amwaacha mashabiki katika tamanio la kuwapa mashabiki kazi mpya kwa jina ‘Nipe Moto’.
Rhino siku kadhaa alieleza kutamani kuachia wimbo mpya, changamoto kubwa yake ya kuchelewa kufanya hivyo ni kutokana na vita ya kupambana na Virusi vya Corona.
Baada ya Post ya madai kuwa Corona ni changamoto, ilifuata post nyingine iliyowekwa kwenye ukurasa wake wa Instagram kwa kitambulishi ‘Hashtag’ cha neno ‘Nipe Moto’.
Hata hivyo kwa kufuatana kwa picha zake mpya na uashiria wa kazi mpya kutoka kwake, Rhino anahisiwa kuwa tayari ameshaingia location kuandaa video ya wimbo ujao.
Kwa sasa Rhino anaendelea kuchanja mbuga za burudani na kufanya vizuri katika chati mbali mbali na wimbo ‘Wekaa’ aliomshirikisha Staa Shetta.




