Msanii wa muziki kutoka nchini Uganda, Douglas Mayanja a.k.a Weasel Manizo amepata mtoto wa kike na Mrembo Sandra Teta, mrembo mwenye asili ya Rwanda.
Weasal akiwa na Mpenzi wake Teta Sandra na Mtoto wao Ria Mayanja
Msanii huyo aliyebaki wa kundi la muziki la nchini humo ‘Goodlyfe Crew’, kupitia ukurasa wa twitter uliwekwa ujumbe kuwa mtoto huyo wa kike aliyezaliwa amepewa jina la ‘Ria Mayanja’.
“Congratulations Teta Sandra | Weasel Sweetlyfe upon your newly born baby STAR MARIA MAYANJA.” Aliandika Jose Chameleone kwenye Ukurasa wake wa Twitter.
Jose Chameleone akifurahia Mtoto wa Weasal
Taarifa zinaeleza kuwa Weasal ambaye ni ndugu wa msanii Jose Chameleone, zinaeleza kuwa baada ya kufanikiwa kupata mtoto huyo, anatimiza idadi ya watoto 28.
Sandra Teta ni mzaliwa wa Kampala Uganda mwenye asili ya Rwanda. Akiwa ni mwenye umri wa miaka 21, mwaka 2013 aliwakilisha nchini ya Rwanda katika mashindano ya urembo, ‘Miss University Africa’.